new_red KARIBU UPAKUE FOMU KWA MAHITAJI MBALIMBALI:new_red MAOMBI YA NAFASI KATIKA SHULE; new_redMirathi / Urithi na Kununua / Kuuza KIWANJA BOFYA HAPA KUZIPATA new_red
Tunamshukuru Mungu kazi ya uinjilishaji imeendelea vizuri ndani ya kanisa kwa kuwatumia watenda kazi wa Kanda na Walezi kwa ukaribu sana. Kila kanda imejipangia ratiba ya kutembelea makanisa katika kanda husika na kwa taarifa za hivi karibuni katika kanda mbalimbali kumefunguliwa matawi mapya. Lengo ni pamoja na kuimarisha makanisa na kufungua matawi mapya baada ya kufikisha ujumbe wa injili ya Yesu Kristo katika maeneo yasiyofikiwa. Kwa upande mwingine, Walezi kwa miaka ya hivi karibuni wameweza kutembelea makanisa karibu yote kwa lengo la kuhimiza ujumbe wa mwaka pamoja na mafundisho ya ziada yaliyofunuliwa kwao kama mafundisho ya kuwa na huruma kwa wenye shida na pia mafundisho ya kulirudisha kanisa katika msingi wa kweli wa "kutubu dhambi za asili, kuziacha, kusamehewa na kutembea katika msamaha" yakiwa ni mafundisho ya msingi toka kwa mwasisi wa UWATA.
Tunamshukuru Mungu kuweza kufikisha injili katika baadhi ya nchi, haiwezi kuwa kazi rahisi lakini Mungu mwenyewe kaifanya. Kuzingatia hilo ofisi ya Katibu Mkuu wa UWATA imeanzisha idara ya mambo ya nje inayo ratibu yanayoendelea katika matawi ya nje ya nchi. Ofisi imekuwa karibu katika kufanikisha usajili wa matawi hayo kutokana na uhitaji wa nyaraka muhimu kwa ajili ya usajili wa kudumu. Tunamshukuru Mungu matawi karibu yote yamepata usajili.
UWATA inayo studio ya kurekodi sauti na video, mradi unaomilikiwa na kuendeshwa na tawi la Bethania-Kanda ndogo ya Dar es salaam kwa uwekezaji wa "Build Operate and Transfer (BOT)". Kwa maelezo zaidi tafadhali bonyeza hapa