new_red KARIBU UPAKUE FOMU KWA MAHITAJI MBALIMBALI:new_red MAOMBI YA NAFASI KATIKA SHULE; new_redMirathi / Urithi na Kununua / Kuuza KIWANJA BOFYA HAPA KUZIPATA new_red
Lengo la awali la UWATA ni kuamsha Wakristo na kila mmoja alalaye dhambini! (Warumi 13:11-14). La pili ni kuhubiri neno la Mungu kwa watu wote na kufanya jitihada (ikiwamo kufundisha, kuhimiza na kushauri) kuhakikisha kwamba matunda (wale walio tubu dhambi na kuziacha) wakae katika utauwa kumsubiri Bwana harusi, Yesu Kristo. Hii imefanikiwa kupitia kukusanyika kila iitwapo leo, (Waebrania 3:13, 10:25). Pia tunatoa huduma mbalimbali katika jamii kama elimu, afya na kushiriki katika utunzaji wa mazingira.
Dira yetu ni kuwa jumuiya ya Kiroho iliyo kimbilio katika kutoa malezi ya KIROHO pamoja na huduma za jamii kama Elimu, Afya na Utunzaji wa mazingira.
Kulingana na Katiba ya UWATA (Toleo la 2012), UWATA inaongozwa na Walezi wakisaidiwa na Bodi ya Wadhamini. Chini ya bodi inafuata Kamati Kuu inayoongozwa na Mwenyekiti wa UWATA. Kamati tendaji ya Kamati Kuu inahusika na uendeshaji wa kila siku wa Jumuiya. Kamati tendaji inaongozwa na Katibu Mkuu wa UWATA, ambaye ni Msemaji na Mtendaji Mkuu wa shughuli za kila siku za UWATA. Chini ya Kamati Kuu kuna Kamati za Kanda na hatimaye Kamati za Matawi. Huo muundo wa uongozi wa jumuiya kutoka ngazi ya Taifa hadi matawini ndiyo unaofanya kazi ya kuongoza kuwa rahisi katika UWATA. Pamoja na hayo, kufuatana na Katiba ya UWATA chombo cha mwisho cha maamuzi ni Mkutano Mkuu ufanyikao mara moja kwa Mwaka,ambao mara nyingi hufanyika kati ya miezi ya Novemba na Disemba. Pia inawezekana muda wowote kufanya Mkutano Mkuu wa dharura / maalumu kama itakavyohitajika.