MWANZILISHI NA ALIYEKUWA MLEZI WA JUMUIYA YA UWATA: MAREHEMU MZEE HARRISONI YESAYA MWAKISWALELE (1920-1991). ALITEMBEA NA YESU MUDA WOTE TANGU ALIPOTUBU NA HATIMAYE KUPUMZIKA KATIKA BWANA.
- Kwa nini napenda kufanya dhambi ambayo siitaki?
Baada ya kubadilika kwa miaka miwili nikajikuta naomba hivi:
- Nifanye nini ili nipate kushinda dhambi?
Baada ya mwaka mmoja kupita nikajikuta naomba hivi:
- Bwana unionyeshe njia, Bwana unionyeshe njia
- Ndipo siku moja nikasikia sauti ikiniambia mwambie Yesu dhambi zako. SIKUIACHIA NAFASI HII IPITE. (Isaya 43:25-26). Ndipo nikaanza kumweleza Bwana dhambi zote nilizozitenda. Baada ya kumweleza yote Bwana wangu niliposema Amen.Nikajikuta nina furaha ya ajabu ambayo sijaiona hata siku moja. Nikasikia sauti ikiniambia; UMESAMEHEWA!!!!
- Siku ya pili nikasikia sauti ikiniambia nenda kawaage makahaba wote ulio tenda nao uzinzi na kurudisha ulivyodhulumu ,ndipo nikafanya hivyo, nikawaaga, nikarudisha, nao wote niliowaibia wengine waliniambia nilipe, wengine walinitangazia msamaha.Nilimshukuru Mungu kwa ukuu wake na rehema zake na huruma kwa wanadamu.
Leo hii UWATA imekua na kufikia hatua ya kuwa na matawi kila kona ya nchi yetu (Tanzania) na katika nchi mbalimbali kama Marekani, Australia, Uingereza, Burundi,Uganda, Kenya, Zambia n.k. Matawi karibu yote katika nchi hizo yamepata usajili wa kudumu. Jumuiya pia inatoa huduma za jamii kama elimu kuanzia hatua ya awali hadi sekondari na chuo; tafadhali tembelea "MIRADI" hapo juu upate taarifa zaidi.